KUONGEZEKA KWA WASANII WAPYA WAMTINGISHA MO MUSIC''MO MUSIC - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, June 2, 2017

KUONGEZEKA KWA WASANII WAPYA WAMTINGISHA MO MUSIC''MO MUSIC

Msanii wa mziki wa kizazi kipya nchini Mo Music amefunguka na kuzungumzia ukimya wake ambao umetokana na kusoma game ya mziki jinsi inavyoenda kwa sasa.

Akizungumza na mtangazaji wa kipindi cha micharazo time cha Dodoma fm amesema aliamua kukaa chini na kusoma game ya mziki kutokana na kutokea kwa wasanii wapya kila kukicha

Hata hivyo msanii huyo amesema yeye kama msanii lazima asome game ya mziki inavyoenda kwa sasa kwasababu sasa hivyi kuna wasanii wengi na wanafanya vizuri ukitofautisha na kipindi yeye anaanza mzikii

''Unajua zamani kipindi mimi naanza mziki hakukuwa na wasaniii wengi kiasi hiki kwahiyo kuna ushindani mkubwa so ndo kitu kilichopelekea mimi nikae kimya na niweze kutafakari ni jinsi gani nitoe ngoma kali zaidi na mashabiki waweze kuupenda mziki wanguu''Alisema Mo music


Ameongeza kuwa mziki umempa mafanikio mengi ikiwepo kumiliki kiwanda cha unga wa sembe kilichopo Mwanza pamoja na kutunza familia yake na sasa hivi ana mpango wa kuanza kusafirisha bidhaa hiyo kwenda mikoani na wiki ijayo bidhaa hiyo itaanza kuuzwa Dodoma

Amewaaidi mashabiki wa mziki wake kuachia kazi yake mpya baada ya mwezi ramadhani na sasa hivi ana kazi saba ambazo zipo tayari

Na Beny Bert  

Social network Beny Bert                                                                      Dodoma

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages