KUNA UTOFAUTI WA KUFANYA MZIKI UKIWA DAR NA DODOMA ''WYSE ONE - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, May 31, 2017

KUNA UTOFAUTI WA KUFANYA MZIKI UKIWA DAR NA DODOMA ''WYSE ONE

Msanii wa mziki wa bongo fleva kutoka Dodoma amesema kuna utofauti mkubwa kwa msanii ambaye anafanya mziki wake akiwa Dodoma na Yule anaye fanya mziki akiwa Dar es salaam.

Akizungumza na Beny Bert mtangazaji wa kipindi cha micharazo time kinachorushwa na Dodoma fm msanii huyo amethibitisha kweli kuna utofauti mkubwa kwa msanii ambaye anafanya mziki akiwa Dodoma ukilinganisha na Yule ambaye yupo Dar es salaam.

Wise one amesema ukiwa Dodoma hata kama una nyimbo mbili unajiona kwamba wewe ni msanii na unajua mziki zaidi ya wenzako na ni vigumu kukutana na changamoto zitazo kufanya ujifunze vitu vingi zaidi katika tasnia ya mziki.


‘’Unajua Dodoma ukiwa pale una vimba mtaani unajiona wewe ndo wewe kiasi kwamba hamna anayeweza kuwa zaidi yako lakini ukiwa Dar kwanza hata kama una nyimbo tatu unajiona bado kwahiyoo unakomaaa ili uwafikie’’Alisema wise one

Kutokana na ukaribu alinao wise one na msanii wa miondoko ya RNB Ben pol  amesema amepata connection nyingi ikiwepo ya kufanikisha kufanya nyimbo na mr,Eazy kutokea nigeria pamoja na Eddy Kenzo wa Ugandaa.

Na Beny  Bert 
Social network  Beny Bert                         

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages