ASTARAVASTE IMENIONYESHA NJIA KWENYE MZIKI WANGU''AZMA MPONDA - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, June 8, 2017

ASTARAVASTE IMENIONYESHA NJIA KWENYE MZIKI WANGU''AZMA MPONDA

Msanii wa mziki wa kizazi kipya Azma Mponda kutoka jiji la mbeya amethibitisha kuanza kuona mafanikio ya muziki wake baada ya kuachia kazi yake inayoitwa ASTARAVASTE  aliyo mshirikisha belle 9 ambayo aliiachia mwishoni mwa mwaka jana.

Akizungumza na Micharazo time ya Dodoma fm radio amesema baada ya kuachia kazi hiyo imemfanya aongeze fan base wengi tofauti na mwanzo ambapo  alikuwa hajulikani.

Kutokana na kuongezeka kwa wasanii wapya kila kukicha ambapo imekuwa changamoto kwa baadhi ya wasanii akiwepo Mo music na kudai ilimlazimu kukaa kimya na kutathmini jinsi gani atarudi kwenye mziki lakini kwa upande wa Azma imekuwa tofauti huku akidai wasanii wapya hawamuumizi kichwa isipokuwa kikubwa ni Connection ya kujuana na watu wengi.

’Unajua katika hii game yetu ya mziki ndio kuna wasanii wengi lakini kikubwa uwe na connection tu hapo inakuwa rahisi sana ya kujuana na watu ili uweze kujulikana kila sehemu’’Alisema Azma

Ameongeza kuwa kiki inaweza ikapelekea msanii kushuka au kupanda kimziki ukitofautisha na msanii ambaye ametoka kwa nguvu zake mwenyewe binafsi kimziki.


Azma anafanya vizuri na wimbo wake Garagasha alio mshirikisha Joseph Mbilinyi maarufu kama sugu pamoja na Izzo bissnes  wote kutoka katika jiji la Mbeya


Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages