MARUFUKU KUKATA TAMAA KWA KIJANA''NANDY - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Sunday, June 4, 2017

MARUFUKU KUKATA TAMAA KWA KIJANA''NANDY

Msanii chipukizi wa mziki wa bongo fleva nchini Nandy amesema hakuwahi kufikiria kama siku moja atapata nafasi ya kutumbiza na wasanii toka nchi mbalimbali Duniani kama ilivyotokea kwake.

Mwanadada huyo ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na kipindi cha  micharazo time cha Dodoma fm radio ambapo amesema kuwa amefurahi kupata nafasi ya kuingia msimu wa Coke studio nchini Kenya 2017 hivyo anaamini ni hatua moja kubwa japo hakuwai kufikiria.

Akizungumzia kuhusu kuhusu experience au uzoefu alioupata coke studio amesema amejifunza jinsi wasanii wa nchi mbali mbali wanavyo fanya kazi zao pamoja na kujali mda.

‘’Unajua ndo mara yangu ya kwanza mimi kuingia Coke studio na sio ishu ndogo ukizungumzia Coke studio ni Dunia unaizungumzia so ni ktu ambacho sikufikiria kama ntakuja siku moja nikutane na wasanii wakubwa kutoka Zimbabwe,Malawi,Nigeria na sehemu zingine kwahiyo nawaambia vijana wenzangu ni mwiko kukata tamaaa kwa sababu hujui kesho yako, kiukweli mi nime hustle miaka mitano lakini sikukata tama na leo hii nimeanza kuona matunda’’Alisema Nandy

Katika hatua nyingine mwanadada  huyo amesema ana kazi yake mpya japo hajaweka wazi amefanya na msanii gani nchini.

Hata hivyo bado anafanya vizuri na wimbo wake unaoitwa   one Day

Story   na  Beny  Bert                                                      Chanzo  Micharazo time

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages