PICHA/STORY BIORN ENTERTIMENT YAKUTANA NA MH MB ANTHONY MAVUNDE, YAWASILISHA CHANGAMOTO NA MAONO YAO KWENYE SANAA YA MUZIKI DODOMA, - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, January 30, 2017

PICHA/STORY BIORN ENTERTIMENT YAKUTANA NA MH MB ANTHONY MAVUNDE, YAWASILISHA CHANGAMOTO NA MAONO YAO KWENYE SANAA YA MUZIKI DODOMA,

Kikundi cha burudani kinacho jishughulisha na sanaa mbalimbali ndani ya mkoa wa dodoma BIORN ENTERTIMENT hivi karibuni imekutana na Mbunge wa Dodoma mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa kazi, vijana na Ajira Mh Anthony Peter Mavunde kwa lengo la kufikisha changamoto zilizopo katika sanaa ya muziki ndani ya mkoa wa Dodoma.
wakiongozwa na mkurugenzi wa BIORN amesema MOH waliweza kufikisha mambo matatu makubwa ambyao wangetamani kuona yanafanyiwa kazi ndani ya sanaa yetu ndani ya mkoa wa dodoma ili sanaa hii iweze kufika mbali zaidi nakutambulika zaidi.

pamoja na mambo ambayo yaliwasilishwa kwa Mh mbunge ni pamoja na kuhakiksha wasanii wa Dodoma wanatumika kama brand kwenye makampuni ambayo yanafanya kazi ndani ya mkoa wa Dodoma, pia kuhakikisha wasanii wadogo wanapata nafasi ya kukutana na wadau wakubwa wa muziki nchini pamoja na kupanua kazi zao kusikika mbali zaidi.

Baada ya kuyapokea hayo Mh mavunde alipata nafasi ya kuzungumza na waliohudhulia kwenye kikao hicho nakusema miongoni mwa vitu ambavyo anatamani kuona ndani ya Dodoma ni kuona Dodoma inakuwa kisanaa na ni miongoni mwa vitu ambavyo ameviwekea kipaombele na tayari ameanza kuvifanyia kazi kwakuunda umoja wa wasanii ambao ni DODOMA KWANZA.;

Aidha amesema kuanzia sasa mtendaji mkuu wa Dom kwanza utaongozwa na yeye mwenyewe ili kupunguza baadhi ya malalamiko yaliyojitokeza mwaka uliopita na tayari ameanza ujenzi wa ofisi ambao unakaribia kukamilika kwani upo kwenye ngazi ya mwisho huko ofisi hiyo ikiambatana na ukumbi mkubwa utakao kuwa ukiwakutanasha wasanii mbalimbali kwaajili ya mazoezi.

pamoja na hayo Mh Mavunde amewataka wasanii wa dodoma kuhakikisha wanabadilika na kuwa wakisasa zaidi ili iwe rahisi wao kusaidiwa kirahisi, "nilazima msanii aonekane vizuri hususani kimuonekano jitambulisho kama msanii ili hata mtu akikuona ajue kuwa wewe kweli ni msanii kuvaa vizuri haijalishi lazima uvae mregezo ushushe suruali hapana nilazima ujitengeneze vizuri uwe msafi na tabia nzuri pia" alisema mh Anthony Mavunde.



Sanajari ana hayo amewapongeza BIORN ENTERTIMENT Kwakuthubutu kunyanyua mziki wa dodoma na kuifanya sanaa ya muzki kuwa ajira kubwa ndani ya moa wa Dodoma.



Na Benedict Ngelangela.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages