MADEREVA WA BAJAJI MANISPAA YA DODOMA WAWALALAMIKIA WASIMAMIZI WA BARABARA - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, December 1, 2015

MADEREVA WA BAJAJI MANISPAA YA DODOMA WAWALALAMIKIA WASIMAMIZI WA BARABARA

Madereva wa bajaji katika halmashauri ya Manispaa ya Dodoma wamelalamikia changamoto ya kusimamishwa ovyo barabarani pindi wanapokuwa katika kazi zao.
Wakizungumza na kituo hiki madereva hao wamesema wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira magumu kwani  suala hilo limekuwa likikwamisha kazi zao.
Kwa upande wake Mwenyekiti mstaafu wa kikundi cha bajaji katika Manispaa ya  Dodoma Bw.Alex Yusuphu amesema kuwa jambo hilo limekuwa likiwapa wakati mgumu kutokana na  vyombo vingine vya usafiri ikiwemo taksi kuwa na mazoea ya kuwachukua abiria wa bajaji .

Pamoja na hayo mwenyekiti huyo amesema wakati mwingine wasimamizi wa barabarani wamekuwa wakiwakwamisha katika kazi hiyo pindi wanapofanya safari zao  kutoka sehemu moja kwenda nyingine


Na Nazael Mkude                                                                        Chanzo:Dodoma FM

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages