JACCO BEAT AELEZA MAMBO YALIYO PELEKEA KUHAMA DODOMA. - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, September 16, 2015

JACCO BEAT AELEZA MAMBO YALIYO PELEKEA KUHAMA DODOMA.

msanii wa kizazi wa kipya toka dodoma wakuitwa JACCO BEATZ baada ya kutokomea kwa muda sasa amerejea na kuzungumza na kituo cha  radio cha 98.4 dodoma fm radio.
jacco beatz na dj mario ndani ya studio za 98.4 dodoma fm radio
JACO BEATZ ambaye ni msanii wa bongo fleva toka mkoani dodoma hivi karibuni aliingia mjini Dar es salaam kimya kimya na kuendelea na harakati zake za muziki.

Akizungumza kupitia kipindi cha Micharazo time toka 98.4 dodoma fm radio kuanzia saa 11 hioni mpaka 2 usiku JACO amesema ameamua kuchukua uwamuzi huo mgumu wa wa kuhamisha makazi lengo likiwa ni kujikuza kisanaa na kujifunza mengi zaidi.

ameongeza na kusema watu wengi wamekua wakitafsiri vibaya maamuzi yake lakini ameweza kufanya hivyo ili kuhakikisha anaongeza ushindani kwa wasanii amabo wapo nje ya dodoma na kujua wanafanya njia gani kujitanua kimuziki pamoja na kusonga mbele kimuziki.

Alipoulizwa ni nini kimemrudisha dodoma kipindi hiki JACO amesema amekuja kufanya kazi za kimuziki za baadhi ya wasanii mkoani hapa pamoja na kusambaza wimbo wake mpya ambao unaitwa Amaizng ambao ameutengeneza yeye mwenyewe..

Kuhusu amejipangaje kumaliza mwaka JACO amesema mashabiki zake watulie vipo vitu vizuri ambavyo ataachia na itakuwa ni balaa kwenye tasnia ya muziki.

Source MICHARAZO TIME YA 98.4 DODOMA FM RADIO.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages