BANZA STONE AKANUSHA TAARIFA ZA KUWA AMEFARIKI DUNIA. - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, June 24, 2015

BANZA STONE AKANUSHA TAARIFA ZA KUWA AMEFARIKI DUNIA.

banza1

Taarifa zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii siku ya jana na leo kuwa msanii wa muziki wa dansi nchini,Banza Stone kuwa amefariki dunia,mwenyewe ameibuka na kukanusha taarifa hizo.
banzaB
Banza amezungumza na Leo Tena ya Clouds Fm, amesema kuwa yeye ni mzima kiafya na alikuwa anaumwa kichwa lakini sasa kimetulia na kwamba taarifa hizo hazijamshtua kwa mara kwa mara amekuwa akizushiwa kuwa amefariki dunia.
‘’Sijafa nipo mzima kiafya na sina tatizo lolote huyo ananizushia kifo aende na mikoa mingine akazushe kuwa nimekufa,’alisema Banza.
Aidha mama Mzazi wa Banza amesema kuwa amekuwa akipigiwa simu nyingi na watu mbalimbali wakimuuliza kama kweli mtoto wake amefariki lakini aliwajibu kuwa ni mzima na hana tatizo lolote.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages