NIKKI WA PILI: MNAOTOA MAANA YA BONGO FLEVA TOENI KIMANTIKI..
Msanii na msemaji wa kundi la wana hip hop (Weusi) kutoka Arusha, Nikki wa II, ameonekana kuto kuridhika na maelezo ya wengine juu ya maana halisi ya neno bongo fleva..
Bongo fleva imekua ikifafanuliwa kama ni ladha inayotoka bongo, hivyo haitofautishi kati ya hip hop na R&B wala aina nyingine ya mziki unaofanywa Tanzania, lakini baadhi ya rappers na wana hip hop kwa ujumla nchini wamekuwa wakilipinga sana hilo hata kuthubutu kuwaita wale wanaoimba ni wabana pua ambao ndio wanaitwa bongo fleva kwa sasa.
siku ya tarehe 16 march, Nikki wa II aliandika maoni yake juu ya hilo kwa kuuliza maswali pia na kutoa hoja yake kupitia katika ukurasa wake wa facebook