YOUNG 60 ALAMBA DUME, NI MSANII WA KWANZA KUSAINISHWA MKATABA WAKUSIMAMIWA NA TEAM SELECTA (DEFARTALITY MUSIC) - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, June 14, 2017

YOUNG 60 ALAMBA DUME, NI MSANII WA KWANZA KUSAINISHWA MKATABA WAKUSIMAMIWA NA TEAM SELECTA (DEFARTALITY MUSIC)

Msanii wa muziki wakizazi kipya YOUNG 60 amekuwa ni msanii rasmi anae simamiwa na team selecta gang ambayo inasimamiwa na Mesen Selecta kutoka Defartality Music.

Image may contain: 1 person, closeup
young 60
Akizungumza na kipindi cha micharazo time toka 98.4 dodoma fm radio YOUNG 60 amesema alikuwa lkakitamani sana kufanya kazi na watu waliopiga hatua kisanaa kwani anaamini kuna changamoto nyingi walizokutananazo na itakuwa rahisi kwake yeye kuelekezwa zaidi ni jinsi gani anaweza kufanya kazi kiusahihi na kwakujiamini zaidi.

60 anasema amekuwa akipata tabu kurekodi nyimbo kwenye studio mbalimbali kwani alikuwa akihitaji kulipia pesa nyingi ambayo kwaupande wake ilikuwa ni changamoto zaidi lakini kwasasa baada yakupata mkataba huo imemrahisishia kurekodi bila mawazo pamoja na kutengenezewa video bila yeye kuchangia chochote na kazi yake kubwa ni kutengeneza mziki mzuri.

pamoja na hayo young 60 amesema mkataba alioupata chini ya defartality music itamsaidia pia kufika mbali kwani wanasimamia promotion za kazi zake zote pamoja na kusambaza ngoma kwenda sehem mbalimbali hadi nje ya TZ

Kuhusu kuhama kundi la Rap Natio 60 amesema mkataba wake hauingiliani na kundi lake kwani kundi lake linamruhusu member yoyote kufanya kazi nje ya kundi bila kufungwa.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages