WAKENYA WAPIGA KURA YA KIHISTORIA - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, March 4, 2013

WAKENYA WAPIGA KURA YA KIHISTORIA

Wakenya wangali wanapiga kura licha ya muda wa mwisho wa shughuli hiyo kutimia.Upigaji kura ulianza asubuhi na mapema baadhi ya wagombea wakiwa katika vituo vya kupiga kura saa nane na saa tisa usiku.
Kulingana na tume ya uchaguzi mkuu, kila mpiga kura ambaye angali kwenye foleni hata baaya ya muda kukamilika, ataruhusiwa kupiga kura, lakini hakuna watu wataruhusiwa kujiunga na foleni kupiga kura.
Baadhi ya vituo vya kupigia kura vimefunga rasmi shughuli ya kupiga kura baada ya muda wa mwisho wa shughuli hiyo kutimia.
Milolongo mirefu ilishuhudiwa katika sehemu nyingi za nchi baadhi zikiwa hata karibu kilomita moja, ishara ya walivyojitokeza wakenya kwa shughuli hiyo ambayo ni ya kihistoria.
Kuna hofu kuwa huenda shughuli hiyo ikaendelea hadi usiku kwani milolongo bado ni mirefu sana.
Kwa hili kuna taarifa kuwa baadhi ya wagombea wanapinga swala la kuendelea na shughuli ya kupiga kura kwa hofu ya wizi wa kura.

Karani wa uchaguzi katika moja ya vituo vya kupigia kura mjini Nairobi

Katika sehemu mbali mbali kulikuwa na visa vya vurugu mfano mjini Mombasa ambako wanachama wa kundi la MRC waliwashambulia polisi waliokuwa wanashika doria na kuwaua wanne.Pia waliwaua raia kadhaa wasiokuwa na hatia.
Lengo la kundi hilo lilikuwa kuvuruga uchaguzi mjini Mombasa pwani ya Kenya.
Kundi hilo limekuwa likitaka uhuru wa jimbo hilo kwa madai kuwa wametengwa na serikali.
Magombea wa urais Raila Odinga aliwataka wananchi kustahimiliana pamoja na kuwapongeza kwa kupiga kura kwa utulivu.
Akina mama waliokuwa na watoto waliruhusiwa kupiga kura bila kupanga foleni

Nae Uhuru Kenyatta alisikitishwa na matukio ya Mombasa na kuwambia wakenya kuwa watulivu pia.
kwa mujibu wa idhaa ya kiswahili ya BBC, foleni mjini Nakuru zimeanza kupungua
Matokeo ya uchaguzi yanatarajiwa kutangazwa leo usiku ingawa tume ya uchaguzi inadai hadi siku saba ili  kutoa matangazo ya matokeo ya kura za urais.

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages