Msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka Dodoma wilaya ya
chemba SMAINA ambaye kwasasa makazi yake ni jijini Dar es Salaam amezungumzia
ujio wa Album yake ambayo itaimbwa kikabila mwanzo hadi mwisho.
Kupitia kipindi cha micharazo Time kutoka 98.4 Dodoma fm
radio, Smaina amesema amebakiza nyimbo mbili tu kukamilisha album hiyo ambayo
itasikika kwa lugha ya kisandawe na amefanya hivo kwa lengo kutukuza asili aliyo
tokea kuwa mzalendo pamoja na kuwapa nguvu vijana wa kisandawe wenye vipaji
kuamini kuwa mambo yanawezekana.
Wiki iliyo pita samaina aliachia wimbo alio washirikisha
wasanii wawili ambao ni Mesen Selekta na Pam D unoitwa Oliva, akizungumza
kufanya kazi hiyo amesema amewashirikisha Mesen na Pam D kwasababu ni watu anao
waamini lakini ni watu wake wa karibu sana.
@benedict_ngelangela
@TonyDvj
@Dodomafmradio