JACO BEAT NDANI YA MGONGO WA MONI CENTRALZONE, UKICHANA MBELEKO SHAURI YAKO. - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, January 18, 2018

JACO BEAT NDANI YA MGONGO WA MONI CENTRALZONE, UKICHANA MBELEKO SHAURI YAKO.

Msanii jaco beatz ameachia wimbo wake hivi karibuni wakuitwa baby ambao kamshirikisha msanii mwenzake anaetokea Dodoma wakuitwa Moni cntralzone anaetamba na wimbo wake wa Mwaaa ft Country Boy, kitu cha kupongezwa kwa hawa vijana ni kuachia wimbo wenye mahudhui mazuri na video kali kiujumla wimbo umejaa vizuri sana.

Sasa hapo kwa wakazi wa Dodoma ishu sio Jaco Beatz kuachia wimbo na Moni maana wote wawili wanafahamika na katia mkoa huu unaweza kuwasimamisha nakuwaweka kwenye meza moja ndio maana watu hawajashtushwa sana Moni kuwekwa kwenye wimbo wa jaco zaidi wamepongezwa kwa kiasi kikubwa kuwa wameungana kupeperusha bendera ya mkoa wao vizuri.
Lakini kwa nje ya mkoa wadodoma huwezi pinga kuwa Moni ni mkubwa sana kuliko Jaco beatz tena kamuacha mbali hawezi kumgusa hata kwenye unyayo kwani Moni anangoma nyingi zimehit hadi nje ya Tanzani nakolabo za wasanii wakubwa kitu ambacho kinamtambulisha Moni kuwa ni msanii wa kitaifa sio msanii wa Kanda Fulani.

Jaco Beatz kufanya kazi na Moni ni jambo la kheri kwakwe kwani kwasasa anaweza kuwanyakuwa mashabiki wa moni wakawa upande wake kwani kuna watu wataupakuwa wimbo kwasababu wameliona jina la Moni Centozone wakaangalia Moni alichofanya ndipo wanapata nafasi ya kumsikia jaco alichoimba kwaio ni credit kwa Jaco beatz.

Pili Moni kwasasa anaconnection ya watu wengi kwaio ni rahisi Moni kumsaidia Jaco kuwafikia wadau wengi wa muziki kwasasa hususani watu waradio na Tv, pamoja na wadau ambao wanaweza kuwapiga tafu kwenye kusambaza ngoma zao,kwaio ni vyema kwasasa Jaco akajinyenyekeza kwa Moni kwani akileta jeuri anaweza akajikuta akirudi nyuma nakukosa msaada ni vyema akutulia nakumuheshimu Moni kama mkubwa kwake kwenye muziki ili nae afikie lengo kwani hata Moni alishawahi kujinyenyekeza kwa watu ndio maana akafikia hapo alipo.

SASA Jaco Beatz mgongo uliobebwa hata kama haukutoshi jishikize hapo hapo sasa ukiruka ruka nakuchana mbeleko hiyo utarudi nyuma na mafanikio utayasikia kwenye Bomba.
TAZAMA VIDEO YAO HAPO.


@ngelangelanews.blogspot.com

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages