KATA YA MLOWA BARABARANI DODOMA HATARINI KUKUMBWA NA TATIZO LA NJAA, DIWANI ATHIBITISHA - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, June 26, 2017

KATA YA MLOWA BARABARANI DODOMA HATARINI KUKUMBWA NA TATIZO LA NJAA, DIWANI ATHIBITISHA

June26,2017                                                                                    Chamwino Dodoma
Wakazi katika Kata ya Mlowa Barabarani Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma wanakabiliwa na changamoto ya upungufu wa akiba ya chakula kutokana na kukosa mavuno ya kutosha katika msimu wa kilimo mwaka 2017.
Image result for NJAA
Diwani wa Kata ya Mlowa barabarani Bw. Alan Nyahan Matheo ameyasema hayo wakati akizungumza na kituo hiki baada ya kufika katika Kata hiyo na kujionea jinsi mazao ya chakula yalivyoungua kutokana na kuchomwa na jua kali hali iliyosababisha wakazi hao kukumbwa na uhaba wa chakula.

Bw. Matheo  amesema changamoto hiyo inatokana na ukosefu wa mvua za kutosha katika msimu wa kilimo mwaka huu hatua iliyochangia kuwepo kwa jua kali lililosababisha mazao ya chakula kukaushwa na kuleta hasara kubwa kwa wakazi wa kata hiyo.

Aidha Bw. Matheo amesema kutokana na changamoto hiyo iliyoikumba Kata ya Mlowa Barabarani uongozi wa kata umelazimika kutoa elimu kwa wananchi juu ya matumizi sahihi ya akiba ya chakula kilichopo ikiwemo kuepuka upikaji wa pombe kwa kutumia mazao ya nafaka.

Hata hivyo Bw. Matheo amesema kwa kuzingatia kauli ya Serikali kuto kutoa chakula cha msaada kwa wananchi wasio jishughulisha imeleta mwamko kwa wakazi wa Kata hiyo kujenga nidhamu ya matumizi sahihi ya chakula cha akiba kilichopo ili kukabilana na changamoto hiyo.



Na PiusJayunga                                                               Chanzo: Dodoma Fm Radio

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages