(AUDIO) SIKILIZA UPAMBANAJI WA MADAWA YAKULEVYA UMEWAKA MOTO DODOMA WAHUSIKA WATAKIWA KJISALIMISHA SEHEMU HUSIKA - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, February 16, 2017

(AUDIO) SIKILIZA UPAMBANAJI WA MADAWA YAKULEVYA UMEWAKA MOTO DODOMA WAHUSIKA WATAKIWA KJISALIMISHA SEHEMU HUSIKA

Siku moja baada ya mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini Bi. Christina Mdeme kuitisha mkutano na wenyeviti wa serikali za mitaa juu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya baadhi ya wenyeviti hao wameahidi kupambana vikali ili kutokomeza vitendo hivyo.
Image result for MADAWA YAKULEVYA
Akiongea na kituo hiki Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa Manispaa ya Dodoma Bw. Matwiga Kiatya amesema kwa kuzingatia agizo la mkuu wa Wilaya wenyeviti wote wa serikali za mitaa katika manispaa ya dodoma wako tayari kupambana ili kutokomeza matumzi ya dawa za kulevya.

Bw. Matwiga amesema ili kutokomeza utumiaji na usambazaji wa dawa za hizo inapaswa kubaini hasa vyanzo vya upatikanaji wake huku mtaa wa Chadulu ukionekana kuwa Mtaa unaoongoza kushamili kwa matumizi ya dawa za kulevya.

Baadhi ya wenyeviti wa Serikali za Mitaa akiwemo Bw. Mohamed Ramadhani kutoka mtaa wa Chidachi pamoja na Bi. Helena Matonya kutoka mtaa wa Mathias Kata ya Miyuji wamekiri kuwepo kwa watu wanaojihusisha na matumizi ya dawa za kulevya katika maeneo yao na kuahidi kuwa wako tayari kuhakikisha vitendo hivyo vinafikia kikomo.

Utekelezaji huo unaanza ikiwa ni agizo la mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini kutoa maelekezo kwa wenyeviti wa serikali za mitaa katika Manispaa ya Dodoma kusimamia zoezi hilo huku mkuu wa jeshi la polisi Wilaya ya Dodoma SSP Daniel Shilaha akitaja baadhi ya Mitaa ambayo inaongoza kwa vitendo hivyo.

sanjari na hayo mwenyekiti wa wenyeviti mkoa wa Dodoma Bw Matwiga kupitia kipindi cha Dodoma live mkoani 98.4 Dodoma fm amesema watumiaji wanatakiwa kujitokeza wenyewe bila kutafutwa na polisi.

Na Pius Jayunga 98.4 dodoma fm radio.




Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages