JAJI SEKIETI KIHIO ASEMA VIONGOZI WATAKIWA KUFUATA SHERIA - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, February 6, 2013

JAJI SEKIETI KIHIO ASEMA VIONGOZI WATAKIWA KUFUATA SHERIA







Jaji Sekieti Kihio
 
Mwanasheria wa mkoa wa Iringa Paul Lekamoi (kulia) akiwa na mwanasheria mwenzake msomi


Mgeni  rasimi kaimu mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dr Leticia Warioba (wa nne kutoka  kushoto) akiwa na majaji na mahakimu  wa mahakamani Iringa wa sita  ni meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi
Baadhi ya  mawakili  mkoani Iringa  wakiwa na mzee  wa matukio  daima wa pili kulia nje ya mahakama kuu leo mara baada ya  maadhimisho ya  siku ya sheria nchini
JAJI  mfawidhi  wa mahakama  kuu ya Tanzania  kanda ya Iringa  Sekieti Kihio amesema  kuwa   wapo baadhi ya  watu wenye mawazo potofu kuwa  Rais wa jamuhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na viongozi  wa  serikali  wapo  juu ya sheria hivyo hivyo  hawapaswi kuzingatia sheria  za nchi jambo ambalo halina  ukweli na kuwa kila mmoja  wetu akiwemo Rais anapaswa  kuzingatia  sheria  mbali mbali na kuheshimu maamuzi ya mahakama.

"Msemo kuwa mfalme  hawezi kutenda  kosa hauna nafasi  katika sheria  zetu  hata kama neno Rais litasimama badala  ya neno mfalme  kila mtu na kila Taasisi  au  shirika katika nchi  hii wote  wanatakiwa  kuheshimu misingi  ya ukuu  wa sheria"

Jaji Kihio  alitoa kauli hiyo leo   wakati wa maadhimisho ya  siku  ya sheria nchini  sherehe zilizofanyika katika  viwanja  vya mahakama  kuu ya Tanzania kanda ya  Iringa na  kuwa suala la utawala  wa sheria  ama upatikanaji  wa  haki  inataka  kuwa  vyombo  vinavyotoa haki  vifikike kwa  wale ambao haki  zao  zimevunjwa  wakiwemo raia ambao haki zao zimeathiriwa na  vitendo  vya  watendaji  mbali mbali wa  serikalini pia  waweze  kudai haki  zao katika  vyombo vinavyotoa haki kwa uhuru  bila woga au upembeleo.

"Sina  Shaka  kuwaeleza  kuwa falsafa  ya mgawanyo  wa madaraka  ya dola ina mahusiano  ya karibu na dhana ya  utawala wa sheria ...serikali  ambayo  imehodhi  mamalaka yote  ya  dola yaani  bunge ,utawala na mahakama  ambayo ina  nia ya  mabavu  itapitisha  sheria yoyote  inayotaka  kama  alivyowahi kusema jaji mkuu  wa Uganda jaji Benjamini J. Odoki  katika mada yake  Uimarishaji wa utawala  wa sheria huko Nairobi April 6 mwaka 2005 katika   moja kati ya kongamano kuwa  serikali  inayohodhi madaraka yote ya dola  itazitumia sheria ilizozipitisha  kinyama  bila  kujali haki na uhuru  wa wananchi  na kama mmoja  wa wananchi anazipinga sheria hizo  serikali  hiyo  itamhukumu bila kujali misingi ya utawala  wa sheria"

Jaji  Kihio alisema  kuwa  bila utawala  wa sheria nchini migogoro ,mivutano ,ushindani  wa kisiasa  na kibiashara  na hata tamaduni vitaendelea kushamiri  na vitapata  suluhu si kwa  njia ya majadiliano bali kwa mabavu ,vitisho  ,kutiana vilema ama kuuwawa ambapo matokeo yake ni amani kutoweka hivyo ili Taifa  liendelee  kuwa na amani ni vema viongozi wa umma kuepuka  kuingilia uhuru  wa mahakama katika  utendaji kazi  wake.

Alisema  kuwa  bila  kuwepo kwa  utawala wa sheria  nchi inaweza  kujikuta ikiingia katika machafuko yasiyokuwa  ya lazima  kwa  vile kila mtu hasa  viongozi  watakuwa  na uhuru  wa kutoa maagizo yoyote ya  kiimla  ili  kusudi  tu  waweze  kutekeleza matakwa yao.

Hata  hivyo  alisema  kuwa kesi nyingi  zinashindwa  kusikilizwa na kumalizika kwa  wakati  kutokana na kiasi kidogo  cha fedha  kinachoingizwa  kwenye  mfuko maalum  wa mahakama na matokeo yake  mahakama  inashindwa  kutoa haki kwa  washtakiwa  kwa  wakati  na hivyo dhana ya  utawala  wa sheria  kutia shaka katika akili  za  wananchi.

Alisema  kuwa  mfano kesi za makosa ya jinai  zinachukua muda  mrefu  kwa sababu ya mashahidi  hawaitwi kutokana na fedha  kwa ajili ya  kuwalipa mashahidi  hao hazipo na hivyo  haki zinacheleweshwa na kupelekea magereza mengi kufurika mahabusu .

Kwa  upande  wake mwanasheria mkuu  wa  serikali kanda ya Iringa Limail Manjoti mbali ya   kuipongeza  tume ya  haki  za  binadamu na utawala  bora  kwa kuendelea kutoa  elimu kwa umma  juu ya hifadhi  ya haki  za binadamu na wajibu  kwa jamii kwa mujibu  wa  katiba ya sheria za nchi  bado alikemea tabia ya  baadjhi ya  vyombo  vya habari na  wanasiasa  kuingilia uhuru  wa mahakama katika  kesi  ambazo bado kutolewa hukumu mafano kesi ya Dowans na TANESCO  kuwa kwa kufanya hivyo ni kuingilia uhuru  wa mahakama.

Kwani  alisema kuwa kufanya   hivyo kunatoa taswira potofu kwa  wananchi hasa  pale maamuzi yatakapotolewa  tofauti  na matarajio ya wengi na kuwa kitendo cha kujadili masuala yaliyopo mahakamani ni  kuingilia uhu
HABARI NA FRANCIS GODWINI

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages