TAHADHARI--UKIKUTANA NA MSG YA NAMNA HII DODOMA JUA NI MATAPELI - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, June 22, 2017

TAHADHARI--UKIKUTANA NA MSG YA NAMNA HII DODOMA JUA NI MATAPELI

                                                           
Wakazi  Mkoani Dodoma wametakiwa kuchukua tahadhari dhidi ya kundi la matapeli lililoibuka na kujitambulisha kwa kutumia simu za mkononi kuwa ni watumishi wa manispaa ya Dodoma huku wakiwatapeli wananchi fedha kwa madai kuwa wanatakiwa kulipia kodi za viwanja na majengo kwa njia ya simu.
Image result for DODOMA
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na afisa habari na uhusiano Manispaa ya Dodoma Bw. Ramadhani Juma inasema kuwa matapeli hao wamekuwa wakitumia vyeo mbalimbali na kutaja gharama ya kodi hizo kuwa ni shilingi elfu 20 hadi elfu 25 kwa kodi za viwanja na majengo

Aidha matapeli hao wamekuwa wakiwataka watu kutuma sehemu ya fedha hizo kwa njia ya simu na kiasi kinachobaki mhusika akiwasilishe katika ofisi za kata husika  kitendo ambacho huwenda kikachafua sifa na uhusiano mzuri baina ya wananchi na watumishi hususani watendaji wa kata na halmashauri

Katika hatua nyingine uongozi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma umeahidi kuendelea kufuatilia kwa karibu wahusika wa vitendo hivyo na hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtu yeyote atakaebainika kuhusika katika vitendo hivyo.


Na Pius Jayunga                                                              Chanzo: Dodoma Fm Radio

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages