Jeshi la Polisi nchini limefanikiwa kuwaua wahalifu wanne
wanaosadikiwa kuwa miongoni mwa wahalifu wanaoendesha mauaji katika
wilaya za Mkuranga, Kibiti na Rufiji katika mapambano yaliyodumu kwa
zaidi ya nusu saa katika kijiji cha Pagae wilayani Kibiti mkoani Pwani.
Akielezea tukio hilo Mkuu wa Oparesheni Maalumu za Jeshi la Polisi,
Naibu Kamishna wa Polisi Liberatus Sabas alisema tukio hilo lilitokea
siku ya Alhamisi juni 29 majira ya saa tatu usiku kwenye barabara ya
vumbi itokayo Pagae kuelekea Nyambunda ambapo Askari Polisi wakiwa doria
walikutana na kikundi cha watu kinachokadiriwa kuwa na watu sita ambapo
wahalifu hao baada ya kuona gari la Polisi walikimbilia vichakani na
kuanza kuwarushia risasi Polisi.
Sabas alisema baada ya hali hiyo kutokea Askari nao kwa ujasiri
walijibu na mapambano hayo yalidumu kwa zaidi ya nusu saa ambapo Polisi
walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu wanne kwa risasi ambao baadaye
walifariki dunia wakiwa wanapelekwa hospitali.
“Katika tukio hilo tumefanikiwa kupata silaha mbili aina ya SMG na
magazine mbili pamoja na risasi 17 zilizokuwa zinatumiwa na wahalifu hao
na hii ni dalili kuwa tunaendelea vizuri na oparesheni yetu ambayo
inashirikisha vyombo vingine vya ulinzi na Usalama katika wilaya hizi
tatu za Mkuranga, Kibiti, na Rufiji” Alisema Sabas.
Aidha Sabas ametoa wito kwa wahalifu wengine kuacha mara moja kufanya
vitendo hivyo kwa kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kufanya
jitihada zote za kuhakikisha kuwa maeneo hayo yanakuwa salama na
wananchi wanaishi katika hali ya amani na usalama.
Vilevile amewataka wananchi kutoa taarifa zitakazowezesha kupatikana
wahalifu wengine ili kuhakikisha kuwa kila mmoja anaishi kwa usalama
ambapo kwa ambaye atakayetoa taarifa zitakazowezesha kupatikana kwa
wahalifu hao kiasi cha shilingi milioni kumi kitatolewa na Mkuu wa Jeshi
la Polisi nchini IGP Simon Sirro.
Post Top Ad
Responsive Ads Here
Friday, June 30, 2017
POLISI WAFANIKIWA KUWAUA WAHALIFU WANNE KIBITI
Tags
# HABARI
Share This
About inngelangelanews.blogspot.com
HABARI
Labels:
HABARI
Post Bottom Ad
Responsive Ads Here
Author Details
Templatesyard is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates which are professionally designed and perfectlly seo optimized to deliver best result for your blog.