MARUFUKU KUCHINJA NGURUWE NDANI YA MKOA WA DODOMA, HOMA YANGURUWE NDIO SABABU - NGELANGELA NEWS

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, June 9, 2017

MARUFUKU KUCHINJA NGURUWE NDANI YA MKOA WA DODOMA, HOMA YANGURUWE NDIO SABABU

Mkuu wa wilaya ya Dodoma Bi Christina Mndeme amepiga marufuku uingizaji na uchinjaji wa nguruwe,kutokana na kuingia kwa mlipuko wa homa ya nguruwe ambao mpaka sasa zaidi ya Nguruwe 200 tayari wameshakufa.
Image result for nguruwe
nyama ya nguruwe

kwaupande mwingine Wafugaji wa nguruwe wametakiwa kufuga ufugaji wa ndani sambamba na  kuacha kulisha nguruwe  mabaki ya vyakula vya binadamu na mizoga ili kuweza kuepuka ugonjwa wa homa ya nguruwe.


Daktari wa mifugo mkoa wa Dodoma Godluck Ndaweka amewatahadharisha wafugaji wa nguruwe kuwa ugonjwa wa homa ya nguruwe hauna tiba hivyo jamii inapaswa kuchukua tahadhari kwa kuzingatia usafi katika mabanda ya nguruwe na kuepuka kuwalisha mabaki ya vyakula vya wanadamu.


Aidha amesema kuwa unaweza kumgundua nguruwe mwenye homa ya nguruwe kupitia dalili mbalimbali ikiwamo  nguruwe kushindwa kula ,kutetemeka sambamba na kuwa na mabaka mekundu sehemu za miguu na mgongoni pia vifo vyao huwa vya ghafla.


Dr Ndaweka amesema pamoja na kwamba ugonjwa wa homa ya nguruwe hauwezi kumpata mwanadamu lakini madaktari wa mifugo hawashauri kutumia kitoweo hicho kwa nguruwe ambao wanaugonjwa huo.


Ugonjwa wa homa ya nguruwe upo mkoani Dodoma  katika halmashauri ya wilaya ya Kongwa,Mpwapwa pamoja na Dodoma mjini ukitokea wilaya ya Gairo mkoani Morogoro hivyo jamii inatakiwa kuchukua tahadhari kwa kutokusafirisha na kuingiza nguruwe sehemu yoyote

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages