Upambanaji wa madawa yakulevya mkoani Dodoma wapamba moto huku wenyeviti wa mitaa wakitakiwa kuhakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kutokomeza madawa yakulevya mitaani. ipo baadhi ya mitaa iliyotajwa kuwa inaongoza kwa vijana wengi kujikita kwenye matumizi ya madawa yakulevya.
Mitaa hiyo nayo ni CHADURU ambayo imeonekana ndiko kwenye tatizo kubwa zaidi ikifutia na kata ya MAJENGO, kata ya MAILI MBILI, kata ya BAHI ROAD pamoja na KIZOTA huko ndiko ambako imeonekana kuwa ni tatizo sugu na mitaa hiyo ilitajwa na mkuu wa jeshi lapolisi mkoa wa Dodoma SSP Daniel Shilaha.
Akiongea na
kituo hiki Mwenyekiti wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa Manispaa ya Dodoma Bw.
Matwiga Kiatya amesema kwa kuzingatia agizo la mkuu wa Wilaya wenyeviti wote wa
serikali za mitaa katika manispaa ya dodoma wako tayari kupambana ili
kutokomeza matumzi ya dawa za kulevya.
Bw. Matwiga
amesema ili kutokomeza utumiaji na usambazaji wa dawa za hizo inapaswa kubaini
hasa vyanzo vya upatikanaji wake huku mtaa wa Chadulu ukionekana kuwa Mtaa
unaoongoza kushamili kwa matumizi ya dawa za kulevya.
Baadhi ya
wenyeviti wa Serikali za Mitaa akiwemo Bw. Mohamed Ramadhani kutoka mtaa wa
Chidachi pamoja na Bi. Helena Matonya kutoka mtaa wa Mathias Kata ya Miyuji
wamekiri kuwepo kwa watu wanaojihusisha na matumizi ya dawa za kulevya katika
maeneo yao na kuahidi kuwa wako tayari kuhakikisha vitendo hivyo vinafikia
kikomo.
Utekelezaji
huo unaanza ikiwa ni agizo la mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini kutoa maelekezo
kwa wenyeviti wa serikali za mitaa katika Manispaa ya Dodoma kusimamia zoezi
hilo huku mkuu wa jeshi la polisi Wilaya ya Dodoma SSP Daniel Shilaha akitaja
baadhi ya Mitaa ambayo inaongoza kwa vitendo hivyo.
sanjari
na hayo mwenyekiti wa wenyeviti mkoa wa Dodoma Bw Matwiga kupitia
kipindi cha Dodoma live mkoani 98.4 Dodoma fm amesema watumiaji
wanatakiwa kujitokeza wenyewe bila kutafutwa na polisi.