MSANII AINEA AMJIA JUU PRODUCER KIMAMBO TOUCH, AMTISHIA KIMAMBO BAADA YA KUDAI KAVUJISHA WIMBO WAKE. - NGELANGELA NEWS

Post Top Ad

Thursday, July 28, 2016

demo-image

MSANII AINEA AMJIA JUU PRODUCER KIMAMBO TOUCH, AMTISHIA KIMAMBO BAADA YA KUDAI KAVUJISHA WIMBO WAKE.

Responsive Ads Here
Kupitia kipindi cha micharazo time cha 98.4 dodoma fm radio kipengele cha DOM.COM amesikika msanii Ainea akilalamika kuwa amevujishiwa wimbo wake na producer wake wakuitwa Kimambo touch.
hqdefault
Ainea amesema alifanya kazi na producer huyo mwaka 2015 mwezi wa pili ambao alimuachia kimambo aendelee kuufanyia mixing kwani hakuwa na haraka ya kuuachia wimbo huo lakini amestushwa kuoona wimbo huo ukiwa umeenea kwenye Blogs mbalimbali.

Ainea ameongeza kwa kusema wimbo ambao umevuja ndio wimbo ambao alikuwa anategemea kuutoa hivi karibuni lakini ameumia zaidi kwani hali hiyo imesababisha kupoteza muelekeo wa kuendelea kupromote wimbo huo.

Alipo ulizwa kuwa ni kwanini ameamua kukimbilia kwenye mitandao ya kijamii, Ainea amejibu sababu yakufanya hivyo ni kutokana na Producer huyo kutopokea simu zake kila akimpigia simu na anashindwa kuchukua hatua zozote kwasababu producer huyo hana studio maalumu.

Mtangazaji wa kipindi cha Micharazo pia alimtafuta producer wa wimbo huo ili kujia ni kwanini wimbo huo umeweza kuwafikia watu bila idhini ya msanii husika, Kimambo amesema hata yeye hafahamu ni nini kimetokea kwani aliibiwa simu mwaka jana akiwepo nchini Kenya(mombasa) na simu hiyo ilikuwa imejaa nyimbo za wasanii mbalimbali kwahiyo anahisi aliye ichukua simu hiyo ndiye alie vujisha wimbo huo.
13567523_1096425380444984_8971436095456882562_n
producer kimambo
kimambo pia amemtaka msanii huyo kuwa mpole na kuangalia ni jinsi gani anaweza kuongeza nguvu kuupromote wimbo huo kwani ni wimbo mzuri ambao unaweza kufanya vizuri.

akijibu ni kwanini ahapokei simu za Ainea, kimambo amesema hutumia muda mwingi kulala kwani hukesha usiku mzima kufanya kazi zake za kimuziki.


Post Bottom Ad

Pages

Contact Form

Name

Email *

Message *