
Akizungumza na Dodoma fm radio kipindi cha Micharazo Time Sadala amesema mwaka 2017 aliacha kuwapa sapoti wasanii wadodoma kwa kuchagua nyimbo zao radioni kutokana na wengi aliokuwa anawasapoti nakufanya kazi walikuwa wanashindwa kurudisha shukrani na mwisho wasiku wamekuwa wakionesha dharau kwa watu wa media tofauti na wasanii wakubwa.
Pamoja na hayo wasanii Sadala amesema kumekuwa na unafki mwingi kwenye game la dodoma kwani watu wameshindwa kuwa wanaambizana ukweli na kuishia kusifiana uongo hata kama kitu hakijakaa sawa hususani upande wa nyimbo.
Sadala anasema ilimuziki wa dodoma ufike mbali ni lazima watu waanze kuambiana ukweli itapunguza kwa idadi kubwa watu wasio na kazi mbovu. "kwa hiyo watu wanafki ni watu wasopenda kusema ukweli"
kwasasa Imma Sadala anamsimamia mwanadada wakuitwa Betty Hizo anae fanya muziki wa hip hop na ameachia wimbo wake wa kwanza unaitwa viulizo.